MINI SHOP CHETA
Mkuu wa wilaya azungumzia barabara ya Magodani, Cheta, Kazole, Kilongoni hadi Vikindu
Aliyasema haya kwenye mkutano wake uliofanyikia tarehe 03/11/2017 eneo la Magodani kisha kuumalizia Kazole, ambapo alisema tayari barabara hii ya kutoka Vikindu hadi Magodani kupitia Kazole na Cheta tayari imeisha wekwa kwenye bajeti na itatengenezwa mda sio mrefu.
![]() |
| Mkuu wa wilaya azungumzia barabara ya Magodani, Cheta, Kazole, Kilongoni hadi Vikindu |
Ambapo alisema atalishugulikia swala hilo baada ya kuwapata walioshiriki kuwauzia raia viwanja hivyo kutoka kwenye eneo la muwekezaji Hamidu.
Kuhusu swala la barabara hii ya Magodani kupitia Cheta, Kazole, Kilongoni hadi Vikindu nitarudi baada ya miezi mitatu 3 ili nione utekelezaji wake umefikia wapi.
CHETA, KAZOLE, MAGODANI, TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI NA KANISA
![]() |
| CHETA, KAZOLE, MAGODANI, TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI NA KANISA |
JINSI YA KUTAMBUA KAMA UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILIWAKO (BODY MASS INDEX BMI)
(BODY MASS INDEX BMI)
Kanuni(BMI)=uzito ÷ (urefu)kipeo cha pili
[ Kg ÷ Meter ÷ Meter ]
BMI ikiwa chini ya 18.50 uzito wako upo chini kuliko kawaida (UNDER WEIGHT).
BMI ikianzia 18.50 hadi 24.99 wewe ni mwenye Afya njema kabisa (HEALTHY).
BMI ikianzia 25.00 hadi 29.99 wewe uzito umezidi (OVER WEIGHT) hivyo uzito wako na urefu wako haviendani kabisa sawa.
BMI ikianzia 30.00 na kuendelea, wewe ni mtu aliyepitiliza kabisa kiwango cha uzito na unaingia katika kundi la (OBESITY).
Tuangalie kwa mfano mimi Muta nina uzito wa Kg 52 na urefu wa Mita 1.65
BMI ya Muta=52÷1.65÷1.65
BMI=19.100
Kwa mfano huo basi Muta yupo kwenye kundi salama maana BMI yake ni 19.100
BAADHI YA MADHARA YA KUWA NA UZITO ULIOZIDI (BMI 25 NA KUENDELEA)
-Magonjwa/matatizo ya Ini na Figo
-Kisukari, Shinikizo la damu, Kiharusi, tatizo la Moyo na magonjwa mengine.
-Kutopumua vizuri wakati wa usingizi
-Kiwango cha juu cha mafuta mabaya
-Ugonjwa wa mifupa kama yabisi
-Matatizo ya hedhi kwa akinamama
-Upungufu wa nguvu za kiume nk.
Vyombo vya habari nchini kutofanya kazi na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam
watanzania mnapoteza muda mwingi kwenye mambo yasiyo ya msingi
tumejielekeza mno kwenye masuala ya udaku ambayo yanatupotezea muda, ambayo hayatupunguzii hata njaa tulizonazo"Rais Magufuli
HABARI NJEMA KWA WAKAZI WA MKOA WA PWANI, NI JUU YA KITUO CHA MABASI KUAMISHIWA MKURANGA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa wilaya za Mkuranga na Temeke, Ofisini kwake jijini Dar es salaam Februari 7, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Moja ya hatua alizowashauri kuchukua ni pamoja na kuhamisha kituo cha mabasi ya mikoa ya kusini ya Lindi, Mtwara na Ruvuma kutoka Temeke hadi Mkuranga.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Februari 7, 2017) alipokutana na viongozi wa wilaya hizo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutafua njia za kuondoa msongamano huo.
Amesema kwa sasa hakuna namna ambayo wataweza kuondoa msongamano huo zaidi ya kuhamishia kituo cha mabasi ya mikoa ya kusini wilayani Mkuranga.
Waziri Mkuu amesema eneo la Mbagala kwa sasa lina msongamano mkubwa ambao ni lazima Serikali ichukue hatua za haraka za kuuondoa.
“Ikiwezekana mabasi ya mikoa ya kusini yaishie Mkuranga, hivyo shirikianeni kutafuta eneo la kujenga kituo kikubwa cha kisasa cha mabasi,” amesema.
Amesema kituo hicho watakachokijenga kiwe na uwezo wa kuhudumia mabasi yote yatokayo mikoa ya kusini na kituo cha Mbagala kiwe cha daladala za kawaida.
Pia Waziri Mkuu amesema kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa kituo hicho kutawezesha kuongeza mapato ya Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga.
Aidha Waziri Mkuu amewataka viongozi hao kwenda kujadiliana katika vikao vya mabaraza ya Madiwani juu ya mkakati huo na kisha kumpelekea taarifa ifikapo Februari 15 mwaka huu.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mkuranga, Bw. Filberto Sanga amesema wazo hilo ni zuri na wilaya yake ina maeneo ya kutosha kujenga miundombinu hiyo.
“Ni kweli wilaya ya Temeke imeelemewa kwa maana ya maeneo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maendeleo na haina pa kupumulia zaidi ya Mkuranga , hivyo tupo tayari kushirikiana nao,” amesema.
Wakati huo huo, Bw. Sanga ameiomba Serikali itakapoanza awamu ya tatu ya ujenzi wa mradi wa mabasi ya mwendo kasi ufike hadi Mkuranga mjini badala ya kuishia Vikindu.
Amesema kwa sasa wilaya yake ina viwanda 67 ambavyo kati yake vipo vinavyofanya kazi na vingine vikiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi, hivyo mabasi hayo yatarahisisha usafiri kwa wafanyakazi.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bw. Felix Lyaniva amesema amefurahishwa sana na mawazo hayo ya kuhamisha kituo cha mabasi cha Mbagala kwani katika vitu vilivyokuwa vinamnyima usingizi ni pamoja na msongamano wa mabasi na wafanyabiashara wadogo wadogo katika eneo hilo.
Makonda na Sirro waitwa Mahakamani leo. Habari kamili iko hapa
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Paul Makonda, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam (ZPC), Kamishna Simon Sirro na Mkuu wa Upelelezi wa kanda hiyo (ZCO), Camilius Wambura, wamepelekewa barua za mwito za kuwataka wafike Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo.
Viongozi hao wamepelekewa mwito huo kutokana na kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe dhidi yao.
Mbowe amefungua kesi hiyo kupinga Makonda kumtaja katika orodha yake ya watuhumiwa 65 wanaojihusisha na dawa za kulevya katika awamu ya pili na kumtaka afike katika Kituo Kikuu cha Polisi, Februari 10 mwaka huu, kwa ajili ya mahojiano.
Katika kesi hiyo Namba Moja ya Mwaka 2017, Mbowe pamoja na mambo mengine, anapinga mamlaka ya RC kumkamata kwa kile anachokiita kudhalilisha watu.
Kesi hiyo imepangwa kutajwa leo na itasikilizwa na jopo la majaji watatu, Sekieti Kihiyo ambaye ni kiongozi wa jopo hilo, akisaidiana na Jaji Lugano Mwandambo na Jaji Pellagia Kaday.
Mbowe anaiomba mahakama hiyo itamke kuwa vifungu vya Sheria ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa vinavyowapa mamlaka wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuwakamata watu na kuwatia mbaroni viko kinyume cha Katiba.
Aidha, Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, jana alifungua maombi mahakamani hapo akipinga kusudio la Kamanda Sirro la kumkamata kama hatajisalimisha katika kituo cha polisi kwa mahojiano.
Mahakama hiyo imetoa hati za mwito wa kufika mahakamani hapo kwa wadaiwa hao ambao ni Makonda, Sirro na Wambura. Hata hivyo, inadaiwa Kamanda Sirro alikataa kupokea mwito huo akielekeza kuwa hati hiyo ya mwito ipelekwe kwa Wambura.
Wadaiwa kukataa kusaini Kwa mujibu wa Ofisa wa mahakama, Yusuph Juma ambaye alipeleka mwito huo, alidai kuwa baada ya kuelekezwa na Kamanda Sirro kuwa ampelekee mwito huo Wambura, alipokwenda kwa Wambura, hakumkuta.
Juma alidai hati ya mwito wa mkuu wa mkoa alipoupeleka hakumkuta na kwamba wasaidizi wake nao walikataa kuusaini mwito huo.
Chanzo: HabariLeo
JE NAULI YA KUTOKA MBAGALA RANGI 3 HADI VIKINDU NI TSH 400 AU 500? SUMATRA TUNAOMBA UFAFANUZI
Magari yote yenye TLB ya kutoa huduma ya usafiri kutoka Temeke hadi Vikindu kupitia Kirwa Road pamoja na yale yote yenye TLB ya Mbagala Rangi tatu hadi Kisemvule, magari haya yamekuwa yakiwatoza abiria wao nauri kubwa kinyume na ile waliyopangiwa kwenye TLB zao.
Mpaka sasa unaposoma habari hii ndugu msomaji wangu nikwamba abiria anayetoka Mbagala rangi tatu hadi Vikindu anatozwa nauri ya Tsh 500 wakati TLB ya gari hilo inamtaka abiria atozwe Tsh 400 pekee.
Lakini pia wale wanaotoka Temeke moja kwa moja hadi Vikindu wao wanatakiwa kulipa Tsh 500 na wale wanaoishia Mbagala walipe 400 na wanao anzia Mbagala hadi Vikindu nao walipe 400 ila hawa wa Mbagala hadi Vikindu hutozwa Tsh 500
Kingine nikwamba unakuta kwenye Tiketi zao wameacha baadhi ya vituo vikubwa, mfano ulio hai tazama tiketi za magari aya utajua ninachokizungumzia, magari aya TLB zake imeandikwa Temeke - Vikindu= 500
Temeke - Mb/Rangi 3= 400
Mb/Rangi 3 - Vikindu =400
Mwanafunzi ni Tsh 200
Ila wao kwenye tiketi zao wameandika
Temeke - Vikindu= 500
Temeke - Mb/Rangi 3= 400
Mwanafunzi 200
Swali ni je kwanini Mbagala hawakuiandika kwenye tiketi zao??
Na kila abilia wakilala mika hawapati msaada, na wakijaribu kuwahoji makondakta wanasema eti Vikindu ipo mkoa mwingine kwaiyo iyo ndio sababu kubwa.
Viongozi wa dini na wamiliki wa hoteli na migahawa, wanaweza kuwa na taarifa zitakazoisaidia polisi
Baada ya awamu ya kwanza kuwalenga wasanii, jana alitaja orodha ya watu 65 iliyohusisha wanasiasa, wafanyabiashara wadogo na wakubwa, viongozi wa dini na wamiliki wa hoteli na migahawa, akisema wanaweza kuwa na taarifa zitakazoisaidia polisi kuwabaini wauzaji wa dawa hizo.
Rais Magufuli apigilia msumari jeneza la wauza Dawa za Kulevya, zaidi ingia hapa
Asema si kazi ya Makonda pekee. Rais Magufulia amesema hakuna wa kuachwa hata akiwa mkewe Mama Janet Magufuli, na kuongeza kuwa wakamatwe bila ya kujali majina yao.
Rais Magufuli amesema anamuomba Jaji Mkuu asizicheleweshe kesi za madawa ya kulevya kwani kuna mtuhumiwa mkubwa wa Dawa za Kulevya anashikiliwa Lindi bila ya kufikishwa Mahakamani.
Najua IGP Mangu watu walikupigia simu wanakupa ushauri kuhusu Dawa za Kulevya, ungewasikiliza leo usingekuwa IGP. Vita ya dawa za kulevya haina cha umaarufu, haijalishi ni mtoto wa nani anahusika, hata kama ni mke wangu mkamateni.
MABADILIKO YA BEI ZA UMEME YALIYOTANGAZWA LEO NA MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA UDHIBITI WA HUDUMA ZA NISHATI NA MAJI (EWURA), FELIX NGAMLAGOSI.
Ifikapo 2017 vituo vyote vya Tv viwe na wakalimani wa lugha ya alama
Katika kuadhimisha ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wenye Ulemavu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama ameagiza vituo vyote vya runinga nchini ifikapo Machi mwaka 2017, kuweka wakalimani wa lugha za alama katika taarifa za habari na matukio ili watu wenye ulemavu wa kusikia wapate habari .
“Ifikapo 2017 vituo vyote vya Tv viwe na wakalimani wa lugha ya alama ili kutekeleza matakwa ya sheria namba 9 hasa katika habari ili walemavu wafuatilie matukio na habari bila ya kuachwa nyuma,” amesema.
Pia amewataka watendaji wa serikali kupanga mipango itakayojibu mahitaji ya watu wenye ulemavu nchini.
Pia ameagiza wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kuwasimamia waganga wakuu kuagiza mafuta ya kuzuia athari za mionzi ya jua kwa watu wenye ulemavu wa ngozi katika Bohari Kuu ya Dawa (MSD).
“Natoa agizo kwa wakurugenzi wa halmashauri nchini wawasimamie waganga wakuu wanapoagiza dawa MSD waagize na mafuta ya kukinga mionzi ya jua dhidi ya ngozi za maalbino, ili kundi hilo lipate mafuta hayo kwa uraisi. MSD pia ijumuishe mafuta ya ngozi katika orodha ya dawa inazoagiza,” alisema.
Pia Mhagama amewaagiza watendaji wa serikali kuunda kamati za watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya kata ili ziratibu changamoto za walemavu kwa ajili ya serikali kutenga bajeti ya kutatua changamoto hizo.
“Watendaji wa serikali waunde kamati za watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya mtaa ili ziweze kujadili changamoto za watu wenye ulemavu. Kamati hizi ziundwe ili bajeti zake ziingie katika bajeti kuu ya serikali,” alisema.
Kuhusu walemavu kupewa msamaha wa matibabu, amesema wizara yake kwa kushirikiana na wizara ya afya inandaa utaratibu wa walemavu kupata huduma ya afya bure bila kubaguliwa.
“Tumekaa na wizara ya afya kuandaa taratibu za walemavu kupata huduma bila kubaguliwa, hivi karibuni changamoto yenu itakwisha,” alisema.
Aidha, amevitaka vyama vya watu wenye ulemavu nchini kuadhimisha siku ya walemavu duniani katika mikoa yote ili kuongeza uelewa kwa wananchi na walemavu kupatiwa stahiki zao.
Asilimia kubwa ya wanawake wanapenda kuwa na wanaume wanaojiweza kiuchumi
POLE MKE WANGU: Rais John Magufuli leo amemtembelea na kumjulia hali mke wake, Mama Janeth Magufuli
Bunge la Tanzania limeridhia msimamo wa Serikali ya Tanzania wa kutokusaini mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi (EPA)

My take:
Nawashukuru sana Wabunge wa Tanzania kwa kuweka Taifa kwanza mbele, na ninashukuru Edward Lowassa na Sumaye waliotia nanga Dodoma kuwafunda wabunge wa UKAWA, matunda yanaonekana.
Naishauri Serikali iache kisainia Mikataba Ikulu. Ni vyema Mikataba yote iwe inapitia bungeni kwa Masilahi mapana ya nchi. Naamini kama Serikali ingekuwa na utaratibu wa kupitisha Mikataba Bungeni, sasa hivi tungekuwa tumeona manufaa ya Madini, gesi na Mafuta.
Msikilize mhe Tundu Lisu akiwasha moto Bungeni juu ya uhuru wa habari nchini.
Kiukweli kabisa tukiachilia mambo ya ushabiki wa vyama, mimi binafsi waga namkubali sana mhe.Tundu Lisu, nimtu anaejielewa kila mda yaani yuko smart antime.
Na leo alikuwa akichangia juu ya mswada wa uhuru wa habari palikuwa hapatoshi bungeni.
===>> BOFYA HAPA KUMSIKILIZA <<===
Bunge laupitisha Muswada wa Huduma za Habari tayari kusainiwa na Rais kuwa sheria. Makosa ya Mwandishi kutokigharimu chombo chake.
RC GAMBO APOKEA MSAADA WA BATI 500 NA MIFUKO YA SARUJI 500
Nteghenjwa Hosseah - Arusha
MKUU wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amepokea msaada wa bati 500 pamoja na mifuko ya saruji 500 kwa ajili ya kuwezesha huduma mbalimbali za maendeleo ikiwemo ujenzi wa zahanati pamoja na shule za msingi na sekondari za Mkoa wa Arusha.
Mara baada ya kukabidhi wa msaada huo nje ya jengo la Ofisi ya Mkuu huyo, Gambo alimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel Dararro mifuko 100 ya saruji na mabati 100 kwa ajili ya ujenzi kituo cha afya kinachojengwa eneo la kwa mama mbauda kata ya Muriet Jijini Arusha.
Alisema msaada huo utawezesha kila wilaya kunufaika nao kwani kila wilaya za mkoa wa Arusha kuna changamoto za uhaba wa vyumba vya madarasa pamoja na mahitaji ya majengo ya zahanati ili kusogeza huduma kwa wananchi.
Alimshukuru Meneja Mradi wa Kampuni ya ujenzi ya Hanil - Jiangsu Joint Venture Ltd, inayojenga barabara ya Sakina - Tengeru Km 14.1 na barabara ya Mchepuko Km 42.4 , Xie Jianbao ambao wametoa msaada huo kama sehemu ya kurudhisha kwa jamii ya watanzania ili kukuza mahusiano na kujali jamii na Taifa ambalo limewapa kazi kubwa ya ujenzi wa barabar hiyo itakayogharimu takribani Bil. 139.
"Naishukuru kampuni hii kwa kutoa msaada huo kwa ajili ya kuleta maendeleo na naahidi tutautumia ipasavyo katika kuleta maendeleo na kila wilaya nitakayofanya ziara msaada huo nitaupeleka ili ya kupunguza changamoto mbalimbali kwa jamii ".
Naye Meneja Mradi wa kampuni hiyo, Bw. Xie alisema kampuni yao imeona umuhimu wa kuchangia jamii kwani wao ni wajenzi wa barabara na wanastahili kurejesha faida kwa jamii inayowazunguka.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe. Gabriel Daqarro alimshukuru Gambo kwa msaada huo na kusisitiza kuwa mifuko hiyo 100 ya saruji pamoja na bati 100 zitasaidia ujenzi wa kituo cha afya kinachojengwa Kata ya Muriet Jijini Arusha.
Naye Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia alishukuru kwa msaada huo utakaosaidia ujenzi wa kituo cha afya kujengwa na kukamilika ndani ya miezi miwili na kuahidi kwamba atasimamia ipasavyo ili kuhakikisha Kituo kinajengwa katia ubora unaostahili.
Katika makabidhiano hayo yaliyohudhuriwa na wabunge wa Viti maalum wanawake Mkoa wa Arusha, Catherine Magige na Aminah Mollel walitoa rai kwa nyakati tofauti kwa wananchi wa mkoa wa Arusha kumuunga mkono Mhe. Gambo pamoja na Serikali ili kuwezesha maendeleo kusonga mbele.































