CHETA, KAZOLE, MAGODANI, TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI NA KANISA

Cheta ni kitongoji kinachopatikana ndani ya kijiji cha Kazole kata ya Vikindu wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.

Maendeleo huletwa na watu, watu wenyewe ndio sisi tukishirikiana na viongozi wetu ndipo tunaweza kupiga hatua chanya kuelekea kwenye kilele cha mafanikio.

Ila wazo ili naona linapingana na uhalisia wa maisha ya wananchi na wakazi wa eneo la Cheta pamoja na viunga vyake.

Ikiwa imepita miezi michache ndani ya mwaka huu wa 2017 tayari zimeonekana alama za vijiti zinazo ashiria njia za uwekaji wa nguzo za umeme.

Alama izo zimetokea eneo la Vikindu zimepita eneo la Kazole mjini, Kazole shule ya msingi iliyopo mpakani na eneo la Hamidu na nguzo ya mwisho imeishia Kazole Magenge 20 eneo la njia panda ya kwenda kwa Bakhresa ambapo ndipo mpakani mwa Kazole na Cheta.

Sasa kuanzia hapo mpakani mwa Cheta na Kazole kwenda hadi mpakani mwa Cheta na Magodani hakuna alama yoyote inayo onyesha kuwa nguzo za umeme zitapita ili kwenda mpaka Magodani.

Cheta ipo ndani ya Kazole uku ikipakana na Magodani ila viongozi wa kazole kwa ujumla wamekuwa wakipasahau sana Cheta.

CHETA, KAZOLE, MAGODANI,  TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI NA KANISA
CHETA, KAZOLE, MAGODANI,  TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI NA KANISA

Baada ya uongozi wa Magodani kuchonga barabara yao kuanzia mpakani mwa Cheta kuelekea kwao ndipo Kazole wao walisimika alama za kuonyesha njia za nguzo za umeme zitakapo pita na wao wakaishia mpakani mwa Kazole na Cheta

Je Cheta inayoachwa katikati inaongozwa na akina nani?? Na je kama ina viongozi wake ivi wao wanatambulika upande wa Magodani au upande wa Kazole?? Wananchi wanataka kufahamu.

Kumbuka wakazi wote wa maeneo ya Mwasonga, Magodani, Cheta, Kazole na Vikindu wanategemea Barabara inayoanzia Vikindu hadi uko Mwasonga pamoja na maeneo mengine ambayo sikuyataja sasa je kama maendeleo na miundo mbinu vinawekwa mwanzoni mwa eneo na mwishoni bila kupaunganisha katikati je kunatengeneza kitugani jamani??

Wananchi wa Cheta wanataka maendelea ya kweli kwa vitendo nasio maendeleo ya kuongea mdomoni na kuwadanganya kwenye mikutano ya vijiji inayofanyika.

Wakazi wa Cheta wanataka Barabara safi, Shule ya msingi na ya Sekondari, Hospital, Soko, Umeme, Visima vya Maji masafi, Viwanja vya Michezo, Sehemu za ibada (Miskiti/Makanisa), Maziko nk.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Desgned By MTM Mikoa Yetu Published.. Blogger Templates
Back To Top