JE NAULI YA KUTOKA MBAGALA RANGI 3 HADI VIKINDU NI TSH 400 AU 500? SUMATRA TUNAOMBA UFAFANUZI

Mimi leo nayasema haya mbele yenu nyinyi wasafiri wenzangu nikiwa na ushaidi wa kutosha kabisa.

Magari yote yenye TLB ya kutoa huduma ya usafiri kutoka Temeke hadi Vikindu kupitia Kirwa Road pamoja na yale yote yenye TLB ya Mbagala Rangi tatu hadi Kisemvule, magari haya yamekuwa yakiwatoza abiria wao nauri kubwa kinyume na ile waliyopangiwa kwenye TLB zao.

Mpaka sasa unaposoma habari hii ndugu msomaji wangu nikwamba abiria anayetoka Mbagala rangi tatu hadi Vikindu anatozwa nauri ya Tsh 500 wakati TLB ya gari hilo inamtaka abiria atozwe Tsh 400 pekee.

Lakini pia wale wanaotoka Temeke moja kwa moja hadi Vikindu wao wanatakiwa kulipa Tsh 500 na wale wanaoishia Mbagala walipe 400 na wanao anzia Mbagala hadi Vikindu nao walipe 400 ila hawa wa Mbagala hadi Vikindu hutozwa Tsh 500

Kingine nikwamba unakuta kwenye Tiketi zao wameacha baadhi ya vituo vikubwa, mfano ulio hai tazama tiketi za magari aya utajua ninachokizungumzia, magari aya TLB zake imeandikwa Temeke - Vikindu= 500
Temeke - Mb/Rangi 3= 400
Mb/Rangi 3 - Vikindu =400
Mwanafunzi ni Tsh 200

Ila wao kwenye tiketi zao wameandika
Temeke - Vikindu= 500
Temeke - Mb/Rangi 3= 400
Mwanafunzi 200

Swali ni je kwanini Mbagala hawakuiandika kwenye tiketi zao??

Na kila abilia wakilala mika hawapati msaada, na wakijaribu kuwahoji makondakta wanasema eti Vikindu ipo mkoa mwingine kwaiyo iyo ndio sababu kubwa.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Desgned By MTM Mikoa Yetu Published.. Blogger Templates
Back To Top