JINSI YA KUTAMBUA KAMA UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILIWAKO (BODY MASS INDEX BMI)

JINSI YA KUTAMBUA KAMA UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILIWAKO
               (BODY MASS INDEX BMI)

Kanuni(BMI)=uzito ÷ (urefu)kipeo cha pili
                    [ Kg ÷ Meter ÷ Meter ]

BMI ikiwa chini ya 18.50 uzito wako upo chini kuliko kawaida (UNDER WEIGHT).

BMI ikianzia 18.50 hadi 24.99 wewe ni mwenye Afya njema kabisa (HEALTHY).

BMI ikianzia 25.00 hadi 29.99 wewe uzito umezidi (OVER WEIGHT) hivyo uzito wako na urefu wako haviendani kabisa sawa.

BMI ikianzia 30.00 na kuendelea, wewe ni mtu aliyepitiliza kabisa kiwango cha uzito na unaingia katika kundi la (OBESITY).

Tuangalie kwa mfano mimi Muta nina uzito wa Kg 52 na urefu wa Mita 1.65

         BMI ya Muta=52÷1.65÷1.65
                         BMI=19.100
Wanangu Diana Mutalemwa Juvenary pamoja na  Allen Mutalemwa Juvenary

Kwa mfano huo basi Muta yupo kwenye kundi salama maana BMI yake ni 19.100

   BAADHI YA MADHARA YA KUWA NA UZITO ULIOZIDI (BMI 25 NA KUENDELEA)

-Magonjwa/matatizo ya Ini na Figo
-Kisukari, Shinikizo la damu, Kiharusi, tatizo la Moyo na magonjwa mengine.
-Kutopumua vizuri wakati wa usingizi
-Kiwango cha juu cha mafuta mabaya
-Ugonjwa wa mifupa kama yabisi
-Matatizo ya hedhi kwa akinamama
-Upungufu wa nguvu za kiume nk.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Desgned By MTM Mikoa Yetu Published.. Blogger Templates
Back To Top