MINI SHOP CHETA

Mini Shop Cheta au Duka Dogo
Mini Shop Cheta logo
Mini Shop logo
Ni duka dogo kweli kama jina lake linavyojieleza hapo juu. Duka hili linatoa huduma ya mahitaji ya kawaida ya kila siku kwa wakazi wa Kitongoji cha Cheta pamoja na maeneo ya jirani au kwa lugha nyingine tunaweza kusema Mini Shop inatoa huduma ya jamii kwa watu wote. Mini Shop ilianzishwa tangu mnamo tarehe 18/01/2018.
Mini Shop Cheta
Mini Shop Cheta
Tulianza tunauza bidhaa chache sana, bidhaa izo ilikuwa ni pamoja na Dawa ya Mbu zile za vidonge za kuchoma, Viberiti, Karanga, Ubuyu pamoja na Tauro za wanawake (Ped). Na kipindi icho tulikuwa tunauza bidhaa izo kutokea nyumbani kabla ya kujenga Frem hii rasmi ya kufanyia biashara kama inavyo onekana hapo kwenye picha.

Mini Shop Cheta Management
Mini Shop Cheta Management
Mini Shop a.k.a Duka Dogo tunauza bidhaa mbali mbali ila kwa ucheche tu, zifuatazo ni baadhi ya bidhaa tunazouza. bidhaa izo zipo chini ya picha hii.
Mini Shop Cheta Map
Mini Shop Cheta Map
Maji
Pipi
Unga
Tambi
Ngano
Amira
Juice
Mikate
Sigara
Chumvi
Mchele
Sukali
Mini Shop Cheta Manager
Mini Shop Cheta Manager

Karamu
Battery
Viwembe
Vitunguu
Viberiti
Biscuits
Madaftari
Vichongeo
Majani ya Chai
Dawa ya Mswaki
Mini Shop Cheta Management finishing
Mini Shop Cheta Management finishing
Jumbo Ball Gum
Sabuni za kuogea
Mafuta ya kupaka
Viungo vya Pirau
Mafuta ya kupikia
Sabuni za kufuria
Maharage ya Njano
Mini Shop Cheta before plaster
Mini Shop Cheta before plaster

Maharage ya Kombati
Tauro za wanawake (Ped)
Pon Pon au Bambino za watoto wachanga
Pia Mini Shop ni wakala wa Vodacom M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
Mini Shop Cheta map Foundation
Mini Shop Cheta map Foundation
Karibu sana dukani kwetu, karibu sana Mini Shop Cheta tukuhudumie leo.

NYUMBA PAMOJA NA FREMU ZA BIASHARA ZINAUZWA

NYUMBA PAMOJA NA FREMU ZA BIASHARA ZINAUZWA

Nyumba hii ina idadi ya vyumba vitano (5) ambavyo unaweza kuvitumia kwenye matumizi yako binafsi kulingana na jinsi unavyotaka kutumia sehemu ya vyumba ivyo.
Cheta kwa Kijonjo

ipo karibu na barabara kuu ya serikari, kwaiyo inafaa sana kwa biashara pamoja na makazi ya kawaida tu ya kila siku kama kulala pamoja na huduma zingine.
Cheta kwa Kijonjo.

tayari imeisha fanyiwa wireling (mfumo wa umeme upotayari) kinachosubiliwa ni umeme kuwashwa tu basi alafu matumizi yaanze.
Cheta kwa Kijonjo frem

Kuhusu huduma ya maji ondoa shaka maana kisima kimechimbwa nyuma ya fremu/nyumba hii, pia eneo iloilo kuna huduma ya tofari, mchanga, cement, kokoto, nk.
Cheta kwa Kijonjo house

Nyumba hii au frem hii, ipo kijiji cha Kazole kitongoji cha Cheta kata ya Vikindu wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani. 

Bei ni tsh 24,000,000/- (millions ishirini na nne) pia mazungumzo yapo.


Mawasiliano:
0659 91 9292







KAMA KWELI UNATAKA KUFANYA BIASHARA PITIA HAPA

Mpenzi msomaji wa makala hii, napenda nikwambie kitu kwamba siku izi watu wengi wanapenda kuanzisha biashara zao binafsi uku lengo lao kuu nikuachana na kuajiliwa kisha wajiajiri wenyewe na kujipatia kipato kupitia biashara zao walizo zianzisha.

Biashara za kufanya ziponyingi sana hapa duniani,ambazo ukizisimamia vizuri zinakutimizia marengo yako.

Mini Shop_Cheta kwa wakala_Mutalemwa

Mbali ya kwamba biashara nyingi zenye faida ya haraka ni zile biashara ambazo zina madhara makubwa kwa afya wa wanadamu mfano waweza kuwa Sigara, Pombe, madawa ya kulevya nk.

Ila zipo biashara ambazo nazo zinakuwa na faida japo kuwa inapatikana taratibu na uchukua mda mrefu kidogo kuonekana tofauti na biasha nilizo tangulia kuzitaja hapo juu.

Biashara izo ni pamoja na Unga wa Sembe, Sukari, mafuta ya kula, Pipi, jojo, soda, maji, madaftari, karamu, nk. Sasa basi, ili uweze kufanikiwa kwenye biashara yako yoyote ile utakayokuwa umeichagua kuianzisha unatakiwa kuwa na mipango mazubuti juu ya usimamizi na uendeshaji wa biashara yako.

Mini Shop+Cheta+kwa wakala+Mutalemwa

Mipango iyo nipamoja na kujua namna ya kutenganisha faida na pesa ya mtaji, kuweza kujua namna ya kuendesha mfumo mzima wa mauzo pamoja na manunuzi, kulipa mishahara nk.

Angalizo, huwezi kufanya biashara bila kumbukumbu, biashara yoyote ile inahitaji utunzaji wa kumbukumbu, usipoweza kipengele hiki basi jua kabisa wewe huwezi kufanya biashara yenye tija, bali unaweza kufanya biashara ya mazoea tu basi. Kujaribu sio kushindwa ebu anza leo uone miujiza ya biashara.

Viwanja vinauzwa kwa bei nafuu sana eneo la Cheta Kazole

Viwanja vinauzwa kwa bei nafuu sana eneo la Cheta_Kazole kata ya Vikindu wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani (Mji unaokua).
          SIFA ZA VIWANJA HIVI
1. Vyote vipo eneo la tambarale, ni umbali wa Futi 320 sawa na Mita 97.55 kutokaka barabara kuu ya serikali.

2. Mchanga unaweza kuchimba kiwanjani mwako hapo hapo.

3. Bomba la maji ya kutumia limepita katikati ya barabara ya mtaa inayopita vilipo viwanja hivi.

4. Viwanja hivi vina urefu wa Futi 50 na upana wa Futi 40 kwa kila kiwanja ikiwa ni sawa na Mita 15.25 kwa mita 12.20

5. Ukubwa wa barabara ya mtaa inayo anzia kwenye barabara kuu ya serikali ina urefu wa Futi 320 na upana wa Futi 16.5 sawa na Mita 97.55 kwa mita 5.

Na ile barabara ya mtaa inayopita viwanjani hapo ina upana wa Futi 10 sawa na Mita 3.5, Pia kuna Futi 2 sawa na Mita 0.60  Zinazotenganisha eneo linalouzwa na eneo la mmiriki.

6. Huduma ya vifaa vya ujenzi kama, Cement, Nondo, Tofari, Mchanga, Kokoto, Maji, vyote vinapatikana jirani kabisa na viwanja hivi vilipo.

Vipo viwanja vinne (4) na kila kiwanja kimoja kinauzwa kwa Tsh. 1.3M (Million 1 na laki 3).
Maongezi yapo kwenye uitaji.

Pia unaweza kulipia kiwanja chako kwa hawamu mbili tu. 

Wote karibuni sana.
Mwenye viwanja naitwa Mutalemwa
Tuwasiliane kupitia 0659 919 292


MAELEZO KUHUSU UMBALI/NAULI
Viwanja hivi vinafikika kwa njia 3 za usafiri.

1. Vikindu kuna stendi ya magari yanayokwenda Kazole magenge 20 na mengine yanakwenda Magodani pia ziko pikipiki (Boda boda).

Kama ukipanda magari yanayoishia Kazole magenge 20 nauri ni Tsh 500 ambapo umbali wa Vikindu to Kazole magenge 20 ni 5.5KM.

Ukishuka hapo kazole utalazimika kutembea umbali wa 2.6KM au kuchukua pikipiki hapo kazole  hadi kufika viwanjani hapo kwa Tsh 1,000

Ila ukipanda magari yanayo kwenda mpaka Magodani nauri yake ni Tsh 1,000 ambapo umbali wa kutoka Vikindu to Cheta kwenye ivyo viwanja ni 8.1KM.

2. Usafiri wa pikipiki kutoka Vikindu to Cheta kwenye viwanja ni Tsh. 3,000

3. Unaweza kutembea kwa mguu kutoka Vikindu hadi Cheta kwenye viwanja hivi kwa mda wa dakika 50-60

Tuwasiliane kupitia 0659 91 9292 au 0787 63 7571

VIWANDA 22 KUJENGWA NCHINI NA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII

VIWANDA 22 vinatarajiwa kujengwa nchini na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, ikiwa ni utekelezaji wa mwito wa Serikali wa kuzitaka hifadhi ya jamii kuwekeza na kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa viwanda nchini.

Katika utekelezaji wa agizo hilo, mifuko ambayo imeshaanza utekelezaji ni NSSF, PPF, PSFP, LAPF, GEPF wakati Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) nao tayari umeanza kufanya mapitio ya kina kwa ajili ya kuwekeza katika uzalishaji maeneo mbalimbali, yenye lengo la kuimarisha upatikanaji wa dawa hospitalini.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (TSSA), Meshack Bandawe alisema jana mjini hapa kuwa hatua hiyo ya mifuko ya hifadhi ya jamii ya kujikita katika uwekezaji wa viwanda, itasaidia asilimia 40 ya ongezeko la ajira nchini itokane na sekta ya viwanda.

Alikuwa akizungumza katika mkutano wa sita wa wadau wa mfuko wa NSSF, unaofanyika mjini hapa.

Katika uwekezaji huo, PPF imeanza mchakato wa ujenzi wa jengo la uzalishaji kwa ajili ya kampuni ya nguo ya TOOKU na kiwanda hicho kinajengwa katika eneo huru la kiuchumi la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Mfuko huo pia utapanua kiwanda cha viatu cha magereza kilichoko Karanga mkoani Kilimanjaro kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza na pia watafanya kwa ubia na NSSF katika kujenga kiwanda cha sukari huko Mkulazi mkoani Morogoro.

Bandawe alisema mfuko wa PSPF utajenga eneo maalumu la kiuchumi katika eneo la Kurasini, ambako kitakuwa ni kituo cha bidhaa zinazotoka China na itajenga kiwanda cha kutengeneza Agave Syrup kutokana na mabaki ya mkonge mkoani Tanga.

Mfuko wa LAPF utafufua Kiwanda cha Chai cha Mponde kilichoko Lushoto, Tanga na watajenga kiwanda cha kutengeneza bidhaa za hospitali na majitiba. Kwa upande wa Mfuko wa GEPF utafanya mradi wa ujenzi na ufufuaji wa kiwanda cha kuchonga vipuri katika eneo la Kilimanjaro Machine Tools mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Mfuko huo pia utajenga machinjio ya kisasa kwa kushirikiana na Kampuni ya Ranchi za Taifa (Narco) na Benki ya Uwekezaji (TIB) huko Tandahimba, Mtwara na kujenga kiwanda cha kusindika juisi na mvinyo utokanao na zabibu huko Chinangali mkoani Dodoma na watafufua na kuendeleza kiwanda cha kubangua korosho cha Tandahimba mkoani Mtwara.

Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (TSSA) wao wamejipanga kufufua na kuendeleza uanzishwaji viwanda vipya vya sekta ya nguo na mavazi, ufufuaji na uendelezaji wa viwanda vipya vya sekta ya ngozi na bidhaa za ngozi na uanzishwaji wa viwanda vipya vya uchongaji wa vipuri.

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara alisema mfuko wake umedhamiria kuwekeza zaidi kwenye viwanda vya kusindika nafaka pamoja na mafuta ya kula.

Aliongeza kuwa uwekezaji katika maeneo hayo, hauhitaji mitaji mikubwa. Alisema kiwanda cha sukari ambacho wanakijenga kwa ubia na PPF, kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 200,000 kwa mwaka na kitatoa ajira kwa watu wapatao 100,000.

Profesa Kahyarara alisema NSSF imejipanga kufufua vinu vya usagaji wa nafaka vya NMC vilivyopo Iringa, Dodoma na Arusha, watafufua kiwanda cha matairi cha Arusha (General Tyre) na pia wanakamilisha uzalishaji wa majaribio wa kiwanda cha viuadudu kilichoko Kibaha, mkoani Pwani.

Mfuko wa NHIF kwa kuanzia unatafanya mradi wa uzalishaji dawa na bidhaa hospitalini, uzalishaji wa maji tiba na uzalishaji wa gesi kwa ajili ya tiba. Kutokana na kujikita katika maeneo hayo, mfuko huo umepanga kufufua viwanda vilivyopo katika hospitali mbalimbali kwa ajili ya utengenezaji wa maji tiba.

Pia watajenga kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za hospitali kwa ubia na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, watajenga kiwanda cha uzalishaji dawa kali kwa ubia na Bohari Kuu ya Dawa (MSD), watajenga kiwanda cha uzalishaji wa gesi ya oksijeni katika Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI).

Bandawe alisema mfuko huo, pia utafanya uwekezaji kwa kushirikiana na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika kufufua uzalishaji wa dawa katika kiwanda cha dawa kinachomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa cha Mgulani; na kujenga kiwanda kipya kikubwa cha kisasa kwa ajili ya kuzalisha dawa pamoja na bidhaa mbalimbali za hospitali katika kambi ya Ruvu.

Alisema mfuko wa ZSSF umejipanga kuingia katika uvuvi wa bahari kuu na usindikaji wa samaki na kuongeza kuwa mfuko huo uko tayari kushiriki katika miradi ya pamoja itakayotekelezwa na TSSA.

“Miradi yote hii tunashirikiana na Benki ya Azania ambayo mifuko yote ni wabia na tunataka kuifanya benki hii iwe ya viwanda. Pia tutashirikiana na JKT katika utekelezaji wa miradi hiyo,” alisema Bandawe.

Wanachama waonesha wasiwasi
Hatua hiyo ya mifuko kwenda kuwekeza kwenye viwanda, imewafanya wanachama wa NSSF kuonesha wasiwasi kama uwekezaji huo utakuwa na tija mbele ya fedha zao. Walitaka kuwepo na maelezo ya kuridhisha, kwa vile mfuko huo unaenda kuwekeza huko wakati kuna manung’uniko ya uwekezaji katika majengo.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi (TUCTA), Gratian Mkoba alipongeza hatua hiyo kwamba inarudisha sasa mashirika ya umma na Serikal kufanya uwekezaji tofauti na miaka ya nyuma serikali ilijiondoa kwenye kufanya biashara.

Samuel Magelo kutoka Tughe alisema ni jambo zuri kuwekeza lakini akahoji inakuwaje mifuko hiyo, inaenda kuwekeza kwenye viwanda huku baadhi yao imeshindwa kulipa mafao ya wanachama wao, kwa madai kuwa haina fedha.

Geofrey Kemeti alisema wadau wanaonesha wasiwasi wa uwekezaji kwenye viwanda na akahoji fedha hizo zitatoka wapi.

“Mifuko yetu itakuwa salama katika uwekezaji huu? Alihoji. SSRA, Profesa Wangwe watetea Katika kujibu hoja hizo, Mwenyekiti wa Bodi ya NSSF, Profesa Samuel Wangwe alisema kwamba bodi ambayo ina dhamana na uwekezaji huo, wamechukua tahadhari kubwa kuhakikisha kwamba uwekezaji utakaofanyika unaongeza mafao ya wanachama. “Kazi yetu ni kulinda fedha zenu, hilo tunalifanya kwa makini. Na bila kuwekeza mafao hayaweza kuongezeka,” alisema Profesa Wangwe.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa mifuko ya hifadhi (SSRA), Irene Isaka alisema kwamba mifuko ina uhuru wa kuwekeza sehemu yoyote ili mradi wafuate mifumo ya uwekezaji. Aliongeza kuwa mifuko inaweza kuwekeza kwa kununua hisa, majengo au kununua hati fungani na kutoa mikopo.

“Tukisema mifuko inaenda kuwekeza kwenye viwanda, sio kwamba fedha zote watazielekeza huko, ni sehemu tu ya fedha itaelekezwa huko,” alisema Irene na kuongeza kuwa uwekezaji kwenye viwanda utaisaidia mifuko kuongeza idadi ya wanachama.

MAJENGO YA SHULE YANAUZWA KWA BEI NAFUU KABISA, HII SI YA KUKOSA JAMANI.

MAJENGO YA SHULE YANAUZWA KWA BEI NAFUU KABISA, HII SI YA KUKOSA JAMANI. 

Majengo ya Shule yanauzwa, majengo ya shule hii yako ndani ya eneo lenye ukubwa wa hekari 3 na robo, majengo ya shule hii yana wastani wa madarasa10, ofisi 3 pamoja na eneo la wazi kwa ajili ya michezo kwa wanafunzi.

Majengo ya Shule hii yako eneo la Picha ya Ndege mkoa wa Pwani karibu na  Kisemvule ikiwa ni 1.1km kutokea barabara kuu ya rami.

Majengo ya Shule hii bado yanajengwa, endapo ukiamua kuyanunua ikiwa kwenye hatua hii kama yanavyo onekana kwenye picha, basi bei yake itakuwa ni Tsh 156millions na bado bei inapungua pia. 

Lakini majengo haya yakimalizika na kupigwa bati juu, Bei yake itakuwa ni Tsh. 200millions, maongezi yapo kwa mteja ambaye yuko tayari kununua (punguzo la bei bado liko pale pale).

Tuwasiliane sasa kupitia namba ya simu ifuatayo hapo mbele (Tigo) 0659 91 9292

Majengo mawili yenye frems 10 yanauzwa, ingia hapa kujua bei

Bado zoezi la kugawa simu linaendelea, ili kushinda simu fuata maelekezo yaliyopo hapo juu. 
Majengo mawili yenye frems 10 za kufanyia biashara, huku kila jengo moja likiwa na frem 5 zenye ukubwa wa kutosha kabisa zinauzwa.
Majengo haya yapo Vikindu ikiwa ni 1km kutoka barabara kuu ya rami.
Majengo haya yote mawili yanauzwa kwa Tsh 150 millions ila maongezi yapo tena mazuri.

Muoneka wa majengo yenyewe ndio kama hivi unavyoyaona.
Ni majengo yaliyo sehemu nzuri sana, tukiachana na kuyasigia kwa sababu yanauzwa.
Muonekano wa barabara inayopita kwenye frems izi, na ukianfalia vizuri kwambele utaziona frems zenyewe ziko upande wa kulia.
Eneo linalozizunguka frems izi ni ilo linalo onekana hapo juu, ukinunua frems izi unakuwa umenunua na eneo lake.
Tuwasiliane kupitia simu namba 0659 91 9292 
Bado zoezi la kugawa simu linaendelea, ili kushinda simu fuata maelekezo yaliyopo hapo chini. 

Majengo ya Nursery School yanauzwa kwa bei nafuu

Tuipende elimu maana ndiyo msingi wa maisha ya mwanadamu.
Majengo ya Nursery school yanauzwa, majengo haya ya shule hii yapo eneo la Chanungu Vikindu mkoa wa Pwani, majengo haya yanawastani wa madarasa saba 7, pamoja na offices 10.
Pia majengo ya shule hii yapo ndani ya eneo la hekari 1 ikiwa ni umbali wa 1km kutoka barabara kuu ya rami mpaka kufika shuleni hapo.
Pia eneo la michezo kwa watoto lipo, majengo hayo yanauzwa kwa bei ya Tsh. 70millions, pia maongezi yapo kama uko serious kununua.
Hii ndio eneo la offices za uongozi wa shule hii, offices zitajengwa kwa mtindo wa ghorofa.

Kama unavyoyaona majengo haya bado hayajakamilika kiujenzi, na huu ndio muonekano wa majengo haya nakumbuka bei inapungua. Tuwasiliane sasa kupitia 0659 91 9292

Nyumba ya kisasa ina vyumba (3) inauzwa, Kufahamu zaidi bofya hapa


Nyumba hii ina vyumba vitatu, ina seating room1, Dining room1, jiko1 
Nyumba hii inapatikana Mbagala Chamanzi Saku. Ukubwa wa eneo la nyumba ni mita 18 upana na urefu ni 20 mita.
Iko ndani ya Fensi, ina umeme, ina matenk ya maji nk. yaani iko full
Inauzwa Tsh 100 millions, lakini maongezi yapo tena mazuri tu!.
Tuwasiliane kupitia 0659 91 9292 
Muonekano mbali mbali wa nyumba hii
Madirisha yake ni yakisasa kabisa kama unavyo yaona hapo kwenye picha.
Muonekano wa sehemu za ndani ya Fensi, pamoja na muonekano wa eneo la chini.

Older Posts
© Desgned By MTM Mikoa Yetu Published.. Blogger Templates
Back To Top