TAMISEMI YAWATAKA WATENDAJI MKOANI ARUSHA KUAXHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA

Tamisemi yawataka watendaji mkoani Arusha kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Naibu waziri wa Tamisemi Bw.Suleimani Jaffo amemtaka katibu  tawala wa mkoa wa Arusha kumpatia orodha ya watendaji   wanaoendelea  kufanya  kazi  kwa  mazoea na kusababisha wananchi   kuteseka  bila  sababu  za  msingi  ili  hatua  zikiwemo za kuwafukuza  kazi zichukuliwe  haraka  kwani  wakati wa kubembelezana umekwisha.

Mh.Jaffo  ameyasema hayo baada ya kupewa taarifa inayopingana na  hali halisi ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali likiwemo la  kushughulikia  maafa yanayowapata wananchi iliyosababisha baadhi ya  watendaji kushindwa  kujieleza na wengine kutupiana lawama na  kuikana  maelezo yao wenyewe.

Mkanganyiko  wa watendaji hao ulikuja baada ya naibu waziri Mh.Jaffo  kutaka kupata maelezo ya  watendaji  hao wanavyoshughulikia  majanga   mbalimbali yanayowapata wananchi likiwemo la kuezuliwa kwa shule  ya msingi isimani lililotokea Desemba mwaka jana ambalo hadi sasa  hatua hazijachukuliwa licha ya kuwa ndani ya uwezo.

Katika sakata hilo kadiri viongozi na watendaji hao walivyojaribu kutoa maelezo yaliendelea  kutofautiana jambo ambalo Mh.Waziri.Jaffo  amesema linalodhihirisha wazi kuwa lipo tatizo ambalo serikali   haiwezi kuendelea kulifumbiwa  macho.

Mh.Naibu waziri Suleiman Jaffo alifanya ziara ya kushtukiza  mkoani  Arusha ambayo inadaiwa kuwa ni matokeo ya malalamiko ya wannachi  wakiwemo wanaopatwa na maafa ama majanga mbali mbali ya  kuchelewa kupata  msaada wa serikali licha ya kupewa ahadi kila janga  linapotokea.  

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Desgned By MTM Mikoa Yetu Published.. Blogger Templates
Back To Top