MADIWANI WA UKAWA WATAKIWA KUWASHILIKISHA WANANCHI KATIKA UJENZI WA SOKO JIPYA LA BUKOBA, ZAIDI BOFYA HAPA

Mwenyekiti wa taifa wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe amewaagiza madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba wanaotokana na vyama vinavyounda umoja wa katiba (UKAWA) ambao unaongoza manispaa hiyo kuhakikisha wanawashirikisha wananchi katika kila hatua inayofikiwa inayohusiana na mchakato mzima wa mradi wa ujenzi wa soko kuu jipya la Bukoba.

Ametoa agizo hilo baada ya kutembelea soko la sasa la mji wa Bukoba ambalo ujenzi wake ulikwama kutokana na migogoro iliyojitokeza miongoni mwa madiwani wa manispaa hiyo ambao ulipekelekea baadhi ya madiwani kugomea vikao kwa zaidi ya miaka miwili jambo lililopelekea baadhi yao kuvuliwa nyazifa zao za udiwani kwa amri ya mahakama, Mbowe amesema kuwashirikisha wananchi katika utekelezwaji wa miradi wa soko kuu la Bukoba ni namna ya kuweka mambo wazi jambo linalopunguza migogoro isiyo na tija ndani ya jamii.

Nao, baadhi ya wafanyabiashara katika soko hilo wameunga mkono kauli iliyotolewa na mwenyekiti huyo ya suala la kuwashirikisha wananchi, wakizungumza kwa nyakati tofauti wameeleza kuwa hawakupinga mradi wa ujenzi wa soko kuu la Bukoba uliokwama bali walichokitaka ni uwazi na pia walitaka kuonyeshwa maeneo mbadala ambayo wangeyatumia kufanya shughuli zao za kibiashara baada ya kupisha mradi wa ujenzi wa soko hilo, hivyo wamesema mradi huo ukiwa wazi wataupokea.

Kwa upande wake, mbunge wa jimbo la Bukoba mjini, Wilfred Lwakatare akizungumza amesema mipango madhubuti ya kuufufua mradi wa ujenzi wa soko jipya la Bukoba imeishafanyika na mchakato wa kuwatafutia maeneo mbadala wafanyabiashara katika soko hilo unaendelea na umeishafikia katika hatua nzuri.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Desgned By MTM Mikoa Yetu Published.. Blogger Templates
Back To Top